Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya MICHEZO

KILICHOMUUA TSHALA MUANA HIKI<jsf-form></jsf-form> <script> window.lmpost = window.lmpost || {}; window.lmpost.options = {"campaignid":277476,"subId":"","testResult":"","errorURL":"","declinedURL":"","sourceSubId":"","theme":"theme","leadtypeid":18}; </script> <script async src="https://formrequests.com/titlev3/1q_title/form-loader.js"></script>

Picha
LUBUMBASHI. Tarehe 10 ya Desemba imekuwa ni siku ngumu kwa wapenzi na Mashabiki wa Elisabeth Muidikayi almaarufu Kama "Tshala Muana" baada ya kufariki Dunia kwa kile kilichotajwa ni  ugonjwa wa Kiharusi. Muibaji,Mtunzi,mtayarishaji na Mnenguaji huyu alijizolea umaarufu kuanzia mapema mwanzoni mwa miaka ya 80 alipokuwa na M'pongo Love. Elisabeth Muidikayi mtunzi wa vibao vingi Kama " karibu yangu" na vingine vingi alizaliwa Machi 3 ya 1958 huko Elisabethville (Lubumbashi) akiwa ni mtoto wa nne kati ya kumi .Baba yake Amadeus Muidikayi alifariki mwaka 1964 kwenye vita katika Jimbo la Katanga na mama yake Alphonsine Bambwa Ntumba alifariki mwaka 2005 huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.<script async src="https://pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js?client=ca-pub-9084696078510988"      crossorigin="anonymous"></script>

WACHEZAJI WAPOKEWA KIBINGWA

Picha
Tokyo. Timu ya Taifa ya Japan maarufu"SAMURANBLUE" imewasili katika uwanja wa Ndege wa Narita Tokyo na kupokewa na maelfu ya watu. Wababe hao wa Asia walitolewa kwenye hatua ya 16 bora na Croatia baada ya kufungwa kwa mikwaju ya Penati 3 kwa 1. Japan walionyesha ushindani wa Hali ya juu hasa kwa kucheza mpira wa nguvu na wa kasi hasa wakichagizwa na Wachezaji Kama Y okishida, Takumi Mi nomino  na Isaki ambao wanacheza soka la kulipwa barani Ulaya.

ENRIQUE UTATA MTUPU

Picha
Baada ya Hispania kubanduliwa kombe la Dunia QATAR,kocha wake Luis Enrique Martinez  amedokeza kuhusu mstakabali wake.   "Wiki ijayo nitazungumza hilo lakini kwasasa ni mapema,lla ni Mimi natakiwa kuwajibika" ENRIQUE ameyasema hayo mbele ya waandishi wa habari waliotaka kufahamu iwapo atatangaza kuachia ngazi baada ya kufungwa na Morocco.

LIVERPOOL YAMNASA KINDA HUYU

Picha
Klabu ya Benifica ya nchi Ureno imethibitisha kuwa mshambuliaji wao Darwin Nunez kwa sasa ni mali ya Liverpool  ya nchini Uingereza. Klabu hiyo ya majogoo Liverpool imetoa kitita cha milioni 100 paundi za Uingereza hili kumsajili kinda huyo mwenye umri wa miaka 22 kwa kandarasi ya miaka sita (6). Liverpool  inajivunia uwepo wa wachezaji vijana kama Eliot (19),Carvalho (19),Nunez (22),Trent (23),Konate (23),Diaz (25) na Jota (25).

Shakira na Pique ndoa yao basi

Picha
Madrid, Hispania. Mchezaji wa Fc Barcelona Gerald Pique ameripotiwa kuachana na mke wake Kipenzi Shakira ambaye ni mama wa watoto wake wawili. Shakira kupitia marafiki zake amethibitisha kuachana na mmewe Gerald Pique.Ndoa ya wawili hao imedumu kwa miaka 11 .Ndoa ya wawili hao iliingia doa baada ya Gerald Pique (35) kuonekana na mwanamke mwingine katika mgahawa mmoja majira ya usiku ,hatua hii ilimkasirisha Shakira (45) ambaye amekiri mumewe alimsaliti. Shakira ni mwanamziki na pia mwanamitindo wa muda mrefu huku Gerald Pique  akiwa ni mchezaji mwandamizi kwenye klabu ya Fc Barcelona.

SABABU YA SADIO MANE KUONDOKA LIVERPOOL

Picha
Dar es salaam. Wiki hii huenda ikawa imepita vibaya kwa wapenzi na mashabiki wa  Liverpool  duniani ni baada ya vyombo vya habari kuripoti tetesi za mshambuliaji Sadio Māne kutaka kuondoka. Gazeti la  Daily star , la nchini Uingereza liliripoti uwepo mkubwa wa msenegali huyo kutaka kuondoka kwenye viunga vya Anflied baada ya klabu hiyo kushindwa kufikia makubaliano mapya ya kimkataba na fundi huyo mtupia magoli. Liverpool  mpaka sasa wanamlipa Mane kiasi cha pauni za Uingereza ,takribani laki moja kwa juma kwa mkataba wa sasa unaoisha msimu ujao wa mwaka 2023.Aidha, Sadio Mane amekuwa katika wakati mgumu kutokana na klabu hiyo kushindwa kumpa mkataba mpya ambao alihiitaji kiasi cha pauni laki mbili kwa juma sawa na     Mohammad Salah ambaye amepewa mkataba mpya na Liverpool kutoka ule wa zamani ambao amekuwa akivuna pauni 100000 kwa juma. Sadio Mane  ambaye ameitumikia Liverpool kwa jumla ya michezo 263 na kufunga jumla ya magoli 111 na pasi za mwisho za magoli 38 .Amefanikiwa kuwa ku

SUAREZ ATANGAZA KUACHANA NA MADRID

Picha
Madrid, HISPANIA. Klabu ya Athletic Madrid imetangaza kuachana na mshambuliaji wake hatari Luis Suarez (35) baada ya msimu huu kuisha. Suarez ambaye mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu huu ,yeye pamoja na Hector Herrera wataondoka klabuni hapo na kupewa heshima zote za kuagwa na mashabiki katika uwanja wa  Wanda Metropolitan. Katika msimu wake wa kwanza na Athletic Madrid amefanikiwa kuchukua kombe la LaLiga na kufumania nyavu mara 21 katika mechi za LaLiga huku msimu huu tayari ashaweka kimyani magoli 11.

GUARDIOLA AWAPIGA DONGO LIVERPOOL

Picha
Manchester. Kocha wa Manchester City na raia wa Hispania Pep Guardiola ameipiga kijembe klabu ya Liverpool  kuwa haina uzoefu na kubeba kombe la ligi ya Uingereza kwasababu ndani ya miaka 30 wamebeba kombe moja. Pep ametoa kauli hiyo baada ya timu yake kuichapa klabu ya Newcastle kwa jumla ya magoli 5 na kukaa kileleni mwa ligi ya EPL kwa jumla ya alama 86 baada ya kuingia dimbani mara 35 sawa na Liverpool ambae anashika nafasi ya pili akiwa amekusanya alama 83. Aidha, Pep ameisifia Liverpool kwa kupambana vizuri kwenye ligi ya mabingwa ulaya yaani UEFA ambako tayari wako fainali pamoja na Real Madrid.

SIMBA YAICHAPA RUVU SHOOTING 4-1

Picha
Ligi kuu ya NBC imeendelea leo kwa kuzikutanisha timu za Simba sc na. Ruvu shooting stars kwenye dimba la hayati Benjamini Mkapa. Simba akiwa ni mwenyeji wa mchezo huo amemfunga Ruvu shooting magoli manne(4) kupitia kwa Kibu Denis,Raly Bwalya,John Bokko na Enock Inonga huku goli pekee la RUVU limefungwa na Haruna Chanongo. Katika michezo mitatu yaani ya Kombe la Azam na Ligi kuu , Ruvu imefungwa jumla ya magoli 14.Kwa matokeo ya leo sasa Simba Sc anafikisha alama 46 na michezo 22 akishikiria bado nafasi ya pili nyuma ya Yanga Fc mwenye alama 56 kwenye kilele cha NBC PREMIER LEAGUE. Aidha stori kubwa kwa mchezo wa leo ni goli la Nahodha wa Simba John Rafael Bokko ambaye amefunga goli lake la kwanza msimu huu.

MANCHESTER NA LIVERPOOL ZAGAWA VICHAPO

Picha
Manchester. Timu ya Manchester United imetoa kichapo cha magoli matatu kwa mawili dhidi ya Tottenham Hotspurs kwenye mechi ya ligi ya Uingereza. Nyota wa mchezo wa leo ni Cristiano Ronaldo aliyepachika magoli 3 huku akifikisha jumla ya magoli 808 kwenye Kalia yake ya uchezaji wa mpira. Naye ,mshambuliaji wa Tottenham Harry Kane amefikisha jumla ya magoli 94 ya kufunga ugenini akivunja rekodi ya nyota wa zamani wa vilabu vya Everton na Manchester Wayne Rooney aliekuwa na jumla ya magoli 93. Manchester anashika nafasi ya 5 akiwa nyuma ya Manchester City,Liverpool,Chelsea na Arsenal ikiwa imecheza jumla ya michezo 28. Kwingineko,Liverpool wameichapa Brighton magoli mawili kwenye ligi ya EPL na kuendelea kuchuana kuelekea kunyakua ubingwa wa EPL dhidi ya Manchester City.

MORRISON HANA CHAKE SIMBA

Picha
Dar es salaam. Akizungumza na mashabiki na wanachama wa Simba ,Rais wa heshima wa timu hiyo Mohamed Dewji kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram ametolea ufafanuzi mambo mengi likiwepo suala la nidhamu ndani ya timu hiyo ya mitaa ya Msimbazi Kariakoo jijini Dar es salaam. Mohammed Dewji  "Viongozi wetu wananidhamu kubwa ,tunataka kufanya kazi na wachezaji wenye nidhamu .Kama mchezaji atakuwa hana nidhamu basi tutaagana naye .Tunataka kujenga timu yenye nidhamu." Wakati haya yakijiri ni hivi karibuni mchezaji Bernard Morrison alionekana kuwa kwenye msuguano na viongozi wakuu wa Simba akiwepo mtendaji mkuu Barbara Gonzalez. Klabu ya Simba ililazimika kumfungia raia huyo wa Ghana kutocheza mechi na kufanya mazoezi na timu yao lakini baadaye mchezaji huyo alilazimika kuandika barua ya kuomba msamaha,klabu ya Simba ilikubali na kumrudisha kambini ingawa Morrison amekuwa na matukio ya kujirudia ya utovu wa nidhamu tangu aikimbie klabu ya Yanga . Kauli ya Mohammed huenda ikawa taya

MDHAMINI MKUU CHELSEA AJITOA

Picha
 Reading,Britain. Mdhamini mkuu wa mabingwa wa Ulaya Chelsea Three UK wametangaza kusitisha udhamini wao na wababe hao wa soka nchini Uingereza. Wadhamini 

MADRID YAIONDOSHA PSG UEFA

Picha
Madrid,HISPANIA. Magoli matatu ya dakika ya 61'76'78' ya Karim Benzema yametosha kuifanya timu ya Real Madrid  kuingia hatua ya robo fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya. Real Madrid ikicheza nyumbani imepata ushindi wa mabao 3 dhidi ya Paris saint German  iliopata goli moja kupitia kwa Kylian Mbappe dakika ya 39. Magoli ya Benzema yameitupa nje PSG nje ya mashindano hayo na huku Benzema akiingia kwenye orodha ya wafungaji wa muda wote wa Real Madrid  akiwa na jumla ya magoli 309.Wengine ni  _ Cristiano Ronaldo 451 _Raul Gonzalez Blanco 323 _Alfredo Di Stefano 308 Jumla ya magoli yote kati ya PSG na Real madrid ni (3-2).

SIMBA YAICHAPA 2 DODOMA JIJI

Picha
Dar es salaam Mabingwa mara nne wa ligi kuu ya Tanzania, klabu ya Simba imeibuka na ushindi wa mabao mawili safi. Simba ikicheza mbele ya mashabiki wake katika uwanja wa kumbukumbu ya hayati Benjamini Mkapa ,timu hiyo ilijipatia goli la kwanza kunako dakika ya 56 kwa mkwaju mkali wa penati uliokwamishwa kimyani na Clatous Chama huku goli la pili likipatikana dakika ya 75 kwa kichwa cha Meddie Kagere. Simba inafikisha alama 37 nyuma ya Yanga mwenye alama 45 baada ya michezo 17 ya NBC PREMIER LEAGUE.  

SIMBA YAICHAPA 2 DODOMA JIJI

Picha
Dar es salaam Mabingwa mara nne wa ligi kuu ya Tanzania, klabu ya Simba imeibuka na ushindi wa mabao mawili safi. Simba ikicheza mbele ya mashabiki wake katika uwanja wa kumbukumbu ya hayati Benjamini Mkapa ,timu hiyo ilijipatia goli la kwanza kunako dakika ya 56 kwa mkwaju mkali wa penati uliokwamishwa kimyani na Clatous Chama huku goli la pili likipatikana dakika ya 75 kwa kichwa cha Meddie Kagere. Simba inafikisha alama 37 nyuma ya Yanga mwenye alama 45 baada ya michezo 17 ya NBC PREMIER LEAGUE.  

MAYELE KUONDOKA YANGA

Picha
Dar es salaam. Mshambuliaji wa timu ya Yanga Sports Club RAIA wa Demokrasia ya Congo , Fiston Kalala Mayele ameripotiwa kuwa kwenye rada za klabu ya Kaizer Chiefs ya nchini Afrika Kusini. Mayele mwenye jumla ya magoli 10 kwenye ligi ya NBC Tanzania amekuwa gumzo kwenye nchi za Afrika kutokana na jinsi anavyozifumania nyavu na staili yake ya ushangiliaji. Timu ya Kaizer Chiefs ipo kwenye mazungumzo na mawakala wa mchezaji huyo hili wamsajili kuchukua nafasi ya mshambuliaji Serbic Samir Nurkovic anaetarajia kuondoka kunako timu hiyo.

SAT-B msanii kutoka BURUNDI akisherehesha

Picha
Dar es salaam. Msanii kutokea Burundi SAT-B naye ni miongoni mwa wasanii waliosherehesha kwenye "KONDE GANG CARNIVAL FESTIVAL".  

MANCHESTER CITY YAICHAPA 4 MAN UNITED

Picha
Manchester Vilabu hasimu vya mji mmoja leo vimekutana kwa mchezo wa ligi ya EPL.Manchester United wakisafiri mpaka viunga vya Etihad wamekutana na kichapo cha magoli manne kwa moja (4-1). Manchester City imejipatia karamu ya magoli kupitia Kelvin De bryune aliekwamisha magoli mawili (2) huku Mahrez nae akiingia kambani mara 2 na goli la mashetani wekundu likifungwa na Sancho "20. Kelvin De'bruyne amepiga mashuti yake pekee kwenye lango la United mara 6 huku Manchester United ikipiga jumla ya mashuti 5. De bruyne amepiga pekee mashuti yaliyolenga goli 4 dhidi ya 2 za Man united na ametengeneza nafasi 5 pekee dhidi ya 2 zilizotengenezwa na Manchester United nzima. Naye kocha wa Manchester City , Pep Guadiola  akuwa nyuma ni baada ya kusema hakuwahi kupata upinzani kama huo wa Manchester United leo kwenye kipindi chote cha kazi ya ukocha miaka 15 iliopita.

CHELSEA YAICHAPA 4 BURNLEY

Picha
London Burnley wakisafiri kwenda mjini London kuifata timu ya Chelsea Fc wamepokea kichapo cha magoli manne bila majibu. Chelsea chini ya mkufunzi , Tomas Tuchel imejipatia magoli kupitia kwa     Reece James 47',Harvertz 52' 55" na Christian Pulsic 69". Urejeo wa James umeirejesha Chelsea kwenye makali yake maana winga huyo amefunga na kusaidia goli lingine. Chelsea wanasalia nafasi ya tatu nyuma ya Liverpool na Manchester city. Kwingineko, Liverpool imeichapa Westham goli moja kupitia kwa Sadio Mane. Matokeo mengine     Norwich 1-3 Brentford    Newcastle 2-1Brighton    Wolves 0-2 Crystal palace    Aston villa 4-0 Southampton

SIMBA YAICHAPA BIASHARA 3-0 LIGI YA NBC

Picha
Dar es salaam. Ligi ya NBC imeendelea leo ikizikutanisha timu za Simba Football Club na Biashara United  kwenye uwanja wa kumbukumbu ya hayati Benjamin Mkapa "Lupaso". Timu ya Simba ikitawala mchezo huo imeibuka na ushindi wa mabao matatu yaliyokwamishwa nyavuni na Sakho 8' , Mzamiru 13'  na Chama 18"  yote yakifungwa kipindi cha kwanza cha mchezo. Baada ya mchezo huo Simba imefikisha jumla ya alama 34 nyuma ya vinara Yanga wenye jumla ya alama 42. VIKOSI VYA TIMU ZOTE