Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari 17, 2022

JINSI YA KUJIPATIA HELA KUPITIA MTANDAO WA FACEBOOK

Picha
BIASHARA. Mtandao wa kijamii wa Facebook ni mmoja ya mitandao mikubwa ya kijamii duniani ukiwa na takribani watumiaji bilioni 4. Mtandao huu unaomilikiwa na kampuni ya META iliopo chini ya bilionea kijana Mark Zuckerberg. Mtandao huu ni miongoni mwa mitandao ya kampuni hii ya META ambayo pia inamiliki Whatsapp ,   Instagram na Messenger. NAMNA YA KUTENGENEZA PESA FACEBOOK Facebook kama ulivyo mtandao wa kibiashara huwa unatoa fursa ya watumiaji wake kunufaika na mtandao huu. Hili utengeneze pesa kwanza fungua 1)  Facebook page: Eneo hili upatikana kwenye kushoto mwa ukurasa wa facebook. -Baada ya kufungua page ,vutia watu kwa kuomba wajiunge na page yako.Page yako itahitaji watu elfu moja (1000) tu hili kuthibitishwa. -Anza kuweka video:Facebook wanalipa kwa video yako tu na wala sio picha,kadri video yako inavyotazamwa ndio huwa unatengeneza pesa ambako watu elfu moja (1k) wakitazama video basi kuanzia hapo video yako itaanza kulipwa.     Mambo ya kuzingatia unapoweka video kwenye Fac

Rais MWINYI APONGEZA TEKNOLOJIA YA KUPIMA CORONA "EDE COVID SCANNER"

Picha
Zanzibar. Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa Zanzibar imekuwa ni nchi ya kwanza Afrika kutumia teknolojia ya mashine ya kupima UVIKO (EDE COVID SCANNERS) kutokana na azma yake ya kuimarisha sekta ya utalii ambayo ndio tegemeo kubwa la uchumi wa Zanzibar  Rais Dkt Mwinyi aliyasema hayo leo wakati akifanya mahojiano na waandishi wa habari wa kimataifa na kitaifa kufuatia matukio makubwa yaliyotokea leo hapa nchini katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume likiwemo kuanza tena kwa safari za ndege ya "Fly Dubai" kutoka umoja wa nchi za kiarabu (UAE) ,pamoja na uzinduzi wa matumizi ya mashine ya (EDE COVID SCANNERS) ya kupima UVIKO 19. Alisema kuwa hatua hiyo itapunguza matatizo ambayo wasafiri wanayapata na kusisitiza kwamba ni muhimu serikali kufanya kila juhudi katika kurudisha watalii hapa Zanzibar ambapo ndege ya "Fly Dubai" itakuwa inakuja mara mbili kwa siku.

KURASA ZA MAGAZETI YA LEO

Picha

DIVA ATANGAZA NDOA YAKE RASMI

Picha
Dar es salaam. Mtangazaji wa kipindi cha LaviDavi kinachoruka kupitia radio ya WASAFI ya jijini Dar es salaam  DivatheeBawse ametangaza rasmi ndoa yake. Kupitia insta story staa huyo aliandika yafuatayo " mume wangu ,halali yangu kabisa @sheikh_abdulrazak_salum .Asante kwa kunioa na kunifanya kuwa mkeo halali kabisa__jamani nakupendaaaaaa sana mume wangu_can't wait for our Nikkah celebration Abdul wangu". Ujumbe wa Diva ulijiri kwenye siku ya Valentine wakati siku hio ikitekwa na tukio la kampuni ya WASAFI kuandaa tukio lilipewa jina la MAHABA. Divatheebawse amejipatia umaarufu mkubwa kupitia Clouds Fm na Wasafi Fm kwa vipindi tofauti tofauti vya mapenzi. Mme wa Diva huyu hapa aitwaye Abdulrazak Salum

SIMBA YAICHAPA RUVU WIKI (7)

Picha
Dar es salaam Timu ya Ruvu shooting  imepokea kipigo cha aibu ni baada ya kukubali kufungwa magoli saba (7) bila majibu na wekundu wa Msimbazi klabu ya Simba Football Club kwenye michuano ya kombe la shirikisho. Mchezo huo wa kufuzu hatua ya robo fainali umechezwa kwenye dimba la Benjamin Mkapa ukishuhudia mvua ya magoli yaliyokwamishwa na John Bocco dakika 01' 39', Clatos Chama dakika ya 23'27'72'', Jimmyson Mwanuke dakika ya 70' na goli la kujifunga la Masinde dakika ya 44". Simba sasa imekuwa timu ya nane (8) kuingia hatua hii baada ya Pamba,Yanga,Kagera,Coastal,Azam na Geita kuwa tayari wamefuzu