SUAREZ ATANGAZA KUACHANA NA MADRID

Madrid, HISPANIA.



Klabu ya Athletic Madrid imetangaza kuachana na mshambuliaji wake hatari Luis Suarez (35) baada ya msimu huu kuisha.

Suarez ambaye mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu huu ,yeye pamoja na Hector Herrera wataondoka klabuni hapo na kupewa heshima zote za kuagwa na mashabiki katika uwanja wa Wanda Metropolitan.

Katika msimu wake wa kwanza na Athletic Madrid amefanikiwa kuchukua kombe la LaLiga na kufumania nyavu mara 21 katika mechi za LaLiga huku msimu huu tayari ashaweka kimyani magoli 11.


Maoni

HABARI KUU LEO

GUARDIOLA AWAPIGA DONGO LIVERPOOL

YANGA NA ARSENAL ZAGAWA DOZI