SABABU YA SADIO MANE KUONDOKA LIVERPOOL

Dar es salaam.



Wiki hii huenda ikawa imepita vibaya kwa wapenzi na mashabiki wa Liverpool duniani ni baada ya vyombo vya habari kuripoti tetesi za mshambuliaji Sadio Māne kutaka kuondoka.

Gazeti la Daily star ,la nchini Uingereza liliripoti uwepo mkubwa wa msenegali huyo kutaka kuondoka kwenye viunga vya Anflied baada ya klabu hiyo kushindwa kufikia makubaliano mapya ya kimkataba na fundi huyo mtupia magoli.



Liverpool mpaka sasa wanamlipa Mane kiasi cha pauni za Uingereza ,takribani laki moja kwa juma kwa mkataba wa sasa unaoisha msimu ujao wa mwaka 2023.Aidha,Sadio Mane amekuwa katika wakati mgumu kutokana na klabu hiyo kushindwa kumpa mkataba mpya ambao alihiitaji kiasi cha pauni laki mbili kwa juma sawa na 


  Mohammad Salah ambaye amepewa mkataba mpya na Liverpool kutoka ule wa zamani ambao amekuwa akivuna pauni 100000 kwa juma.

Sadio Mane 


ambaye ameitumikia Liverpool kwa jumla ya michezo 263 na kufunga jumla ya magoli 111 na pasi za mwisho za magoli 38 .Amefanikiwa kuwa kutwaa mataji ya klabu bingwa Ulaya ,klabu bingwa ya Dunia,Ligi kuu ya Uingereza na makombe ya FA na Carabao yote ya nchini Uingereza. Msimu huu pekee Sadio Mane amefunga magoli 16 ndani ya ligi kuu ya soka Uingereza na pia jumla ya magoli 5 kwenye klabu Bingwa ya Ulaya.

Mpaka sasa vilabu vya Bayern Munich ,Juventus na Paris Saint German vimeonyesha kuhitaji huduma yake mwamba huyo wa soka la Africa.

Maoni

HABARI KUU LEO

GUARDIOLA AWAPIGA DONGO LIVERPOOL

YANGA NA ARSENAL ZAGAWA DOZI