Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya HABARI KUU

KILICHOMUUA TSHALA MUANA HIKI<jsf-form></jsf-form> <script> window.lmpost = window.lmpost || {}; window.lmpost.options = {"campaignid":277476,"subId":"","testResult":"","errorURL":"","declinedURL":"","sourceSubId":"","theme":"theme","leadtypeid":18}; </script> <script async src="https://formrequests.com/titlev3/1q_title/form-loader.js"></script>

Picha
LUBUMBASHI. Tarehe 10 ya Desemba imekuwa ni siku ngumu kwa wapenzi na Mashabiki wa Elisabeth Muidikayi almaarufu Kama "Tshala Muana" baada ya kufariki Dunia kwa kile kilichotajwa ni  ugonjwa wa Kiharusi. Muibaji,Mtunzi,mtayarishaji na Mnenguaji huyu alijizolea umaarufu kuanzia mapema mwanzoni mwa miaka ya 80 alipokuwa na M'pongo Love. Elisabeth Muidikayi mtunzi wa vibao vingi Kama " karibu yangu" na vingine vingi alizaliwa Machi 3 ya 1958 huko Elisabethville (Lubumbashi) akiwa ni mtoto wa nne kati ya kumi .Baba yake Amadeus Muidikayi alifariki mwaka 1964 kwenye vita katika Jimbo la Katanga na mama yake Alphonsine Bambwa Ntumba alifariki mwaka 2005 huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.<script async src="https://pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js?client=ca-pub-9084696078510988"      crossorigin="anonymous"></script>

KURASA ZA MBELE ZA MAGAZETI LEO

Picha
Dar es salaam. Hujambo Mtanzania, Alhamisi ya leo?

ENRIQUE UTATA MTUPU

Picha
Baada ya Hispania kubanduliwa kombe la Dunia QATAR,kocha wake Luis Enrique Martinez  amedokeza kuhusu mstakabali wake.   "Wiki ijayo nitazungumza hilo lakini kwasasa ni mapema,lla ni Mimi natakiwa kuwajibika" ENRIQUE ameyasema hayo mbele ya waandishi wa habari waliotaka kufahamu iwapo atatangaza kuachia ngazi baada ya kufungwa na Morocco.

AFRIKA YAWEKA HISTORIA QATAR

Picha
Timu ya Morocco imekuwa timu ya Afrika mwaka 2022 kutinga robo fainali ya kombe la Dunia QATAR akiwafunga Hispania kwa mikwaju ya Penati. Mchezo huo ambao umedumu kwa takribani dakika 120 na nyongeza 8 umetamatika kwa Waarabu hao wa Kaskazini mwa Afrika kutakata kwa kuibandua Spain kwa mikwaju 3 bila majibu. Kijana aliezaliwa Madrid ndiye amekuwa gumzo kwa kushindilia mkwaju mkali wa mwisho wa Penati huku kipa wa Morocco akicheza mikwaju yote ya Marco Asensio,Laporta na nahodha wa Uhispanyola Sergio Busquet. Morocco atamsubiri mshindi kati ya Ureno na Uswizi hili atafute tiketi ya kwenda nusu fainali.

LIVERPOOL YAMNASA KINDA HUYU

Picha
Klabu ya Benifica ya nchi Ureno imethibitisha kuwa mshambuliaji wao Darwin Nunez kwa sasa ni mali ya Liverpool  ya nchini Uingereza. Klabu hiyo ya majogoo Liverpool imetoa kitita cha milioni 100 paundi za Uingereza hili kumsajili kinda huyo mwenye umri wa miaka 22 kwa kandarasi ya miaka sita (6). Liverpool  inajivunia uwepo wa wachezaji vijana kama Eliot (19),Carvalho (19),Nunez (22),Trent (23),Konate (23),Diaz (25) na Jota (25).

Shakira na Pique ndoa yao basi

Picha
Madrid, Hispania. Mchezaji wa Fc Barcelona Gerald Pique ameripotiwa kuachana na mke wake Kipenzi Shakira ambaye ni mama wa watoto wake wawili. Shakira kupitia marafiki zake amethibitisha kuachana na mmewe Gerald Pique.Ndoa ya wawili hao imedumu kwa miaka 11 .Ndoa ya wawili hao iliingia doa baada ya Gerald Pique (35) kuonekana na mwanamke mwingine katika mgahawa mmoja majira ya usiku ,hatua hii ilimkasirisha Shakira (45) ambaye amekiri mumewe alimsaliti. Shakira ni mwanamziki na pia mwanamitindo wa muda mrefu huku Gerald Pique  akiwa ni mchezaji mwandamizi kwenye klabu ya Fc Barcelona.

SABABU YA SADIO MANE KUONDOKA LIVERPOOL

Picha
Dar es salaam. Wiki hii huenda ikawa imepita vibaya kwa wapenzi na mashabiki wa  Liverpool  duniani ni baada ya vyombo vya habari kuripoti tetesi za mshambuliaji Sadio Māne kutaka kuondoka. Gazeti la  Daily star , la nchini Uingereza liliripoti uwepo mkubwa wa msenegali huyo kutaka kuondoka kwenye viunga vya Anflied baada ya klabu hiyo kushindwa kufikia makubaliano mapya ya kimkataba na fundi huyo mtupia magoli. Liverpool  mpaka sasa wanamlipa Mane kiasi cha pauni za Uingereza ,takribani laki moja kwa juma kwa mkataba wa sasa unaoisha msimu ujao wa mwaka 2023.Aidha, Sadio Mane amekuwa katika wakati mgumu kutokana na klabu hiyo kushindwa kumpa mkataba mpya ambao alihiitaji kiasi cha pauni laki mbili kwa juma sawa na     Mohammad Salah ambaye amepewa mkataba mpya na Liverpool kutoka ule wa zamani ambao amekuwa akivuna pauni 100000 kwa juma. Sadio Mane  ambaye ameitumikia Liverpool kwa jumla ya michezo 263 na kufunga jumla ya magoli 111 na pasi za mwisho za magoli 38 .Amefanikiwa kuwa ku

KOFFI OLOMIDE AKUBALI UJIO WA WENGE

Picha
Kinshasa DRC Mwanamziki mkongwe barani Afrika Charles Antonio Mumba Olomide amefurahishwa na hatua ya wanamziki waliounda kundi la  WENGE MUSICA au WENGE MUSICA BCBG kuamua kuungana upya katika hatua ya kufufua kundi hilo.Kundi la WENGE MUSICA lilianzishwa na Didier Msika mwaka 1981 likipitia tena kwenye mikono ya JB MPIANA mnamo mwaka 1986 kablà ya kuvunjika mwaka 1997 huku sababu ikitajwa viongozi wake wakuu kutoelewana. Nguli huyu wa miondoko ya Sokous na Rhumba amesema anapenda kundi hili lirudi upya huku akizungumzia kile ambacho huwa kinatajwa kwamba yeye na Papa Wemba ndio walikuwa watu waliosababisha kundi hilo kufa amesema nafurahi sana WENGE MUSICA kurudi lakini mimi nilisemwa kuliua kundi hili lakini hiyo ilikuwa vita ya ushindani Wa kimziki na kutafuta ufalme pia wa mziki .

HISTORIA YA MAISHA YA PAPA WEMBA

Picha
Mwanamziki Papa Wemba alizaliwa 14 Juni 1949 na kufariki 24 April 2016,alizaliwa Lubefu Zaire ya Zamani. Papa Wemba ni mwamba Wa Mziki Wa Sukus na anafahamika Dunia kwa mtindo wake Wa uvaaji na utanashati ujulikanao kwa lugha ya Kifaransa yaani la Saperé. Umaarufu zaidi Wa Papa Wemba ulitokana na kundi lake la mziki la Viva la Musica  Mwaka 1969,Papa Wemba akiwa na hakina Nyoko Longo,Bimi Ombale,Moloko Leilei na Vuela Somo walikuwa vijana wa mwanzo watanashati na walijiunga na kuanzisha kundi la mziki la Zaiko Langa langa lililokuwa likiimba mziki Wa Sukusi.Tofauti ya mziki wa Sukusi na Rhumba la wakati huo wa makundi ya TP OK Jazz au Afriza International  ni kwamba mziki huu unaenda kasi mno.Mziki huu ulianzishwa na vijana waliochoshwa na mziki wa Rhumba wa kukumbatiana mwanzo mwisho bila jasho ,wao walitaka toka nukta ya kwanza ya kuanza mziki ni kucheza mwanzo mwisho. Sukusi  ni kizazi cha nne cha mziki wa Rhumba kutoka Zaire,utamaduni waliopitia vizazi vinne na kuunda kile kizazi k

GUARDIOLA AWAPIGA DONGO LIVERPOOL

Picha
Manchester. Kocha wa Manchester City na raia wa Hispania Pep Guardiola ameipiga kijembe klabu ya Liverpool  kuwa haina uzoefu na kubeba kombe la ligi ya Uingereza kwasababu ndani ya miaka 30 wamebeba kombe moja. Pep ametoa kauli hiyo baada ya timu yake kuichapa klabu ya Newcastle kwa jumla ya magoli 5 na kukaa kileleni mwa ligi ya EPL kwa jumla ya alama 86 baada ya kuingia dimbani mara 35 sawa na Liverpool ambae anashika nafasi ya pili akiwa amekusanya alama 83. Aidha, Pep ameisifia Liverpool kwa kupambana vizuri kwenye ligi ya mabingwa ulaya yaani UEFA ambako tayari wako fainali pamoja na Real Madrid.

SIMBA YAICHAPA RUVU SHOOTING 4-1

Picha
Ligi kuu ya NBC imeendelea leo kwa kuzikutanisha timu za Simba sc na. Ruvu shooting stars kwenye dimba la hayati Benjamini Mkapa. Simba akiwa ni mwenyeji wa mchezo huo amemfunga Ruvu shooting magoli manne(4) kupitia kwa Kibu Denis,Raly Bwalya,John Bokko na Enock Inonga huku goli pekee la RUVU limefungwa na Haruna Chanongo. Katika michezo mitatu yaani ya Kombe la Azam na Ligi kuu , Ruvu imefungwa jumla ya magoli 14.Kwa matokeo ya leo sasa Simba Sc anafikisha alama 46 na michezo 22 akishikiria bado nafasi ya pili nyuma ya Yanga Fc mwenye alama 56 kwenye kilele cha NBC PREMIER LEAGUE. Aidha stori kubwa kwa mchezo wa leo ni goli la Nahodha wa Simba John Rafael Bokko ambaye amefunga goli lake la kwanza msimu huu.

MOZEY BROWN AACHIA WIMBO WAKE"MAMA LAO"

Picha
Dar es salaam. Msanii wa kizazi kipya Moses Joseph ameachia wimbo wake mpya ujulikanao kama MAMA LAO ambao kwasasa unapatikana kwenye mitandao ya kijamii kama YouTube, Audiomack,Boomplay,na Facebook. Meneja wa msanii huyo Mujuni Henry ,amethibitisha hilo rasmi kwenye ukurasa wake wa kijamii wa Instagram huku pia kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook. Mpaka sasa wimbo huo unaendelea kufanya vizuri huku pia mashabiki wa mziki wa bongo fleva wakikiri kuwa msanii MOZEY BROWN anafuata nyayo za wasanii wa muda mrefu kwenye kiwanda cha mziki wa Tanzania yaani Bongo Fleva. MOZEY BROWN ni nani? Ni msanii wa mzazi kipya ambaye kwa sasa ameingia kwenye mziki kwa mara ya kwanza na akiwa ametoa wimbo wake huo mmoja wa " MAMA LAO" . Ni mkaazi wa jiji la biashara la Dar es salaam akiwa chini ya management ya mfanyabiashara MUJUNI HENRY.

DIAMOND NA ZUCHU WAPATA PIGO

Picha
Dar es salaam. Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) imezuia wimbo wa Diamond ft Zuchu ujulikanao kama "mtasubiri" kwa muda kutokana na kipande cha video kuonekana na tafsiri mbaya. Katika taarifa ya mamlaka hiyo nchini imeeleza video ya wimbo huo ina kipande kinachoonyesha Zuchu ni mwana kwaya ambaye yuko kanisani anaimba na ghafla anapigiwa simu na kupokea simu wakati anaimba kwenye kwaya. Kutokana na kitendo hicho kipande, hali imekuwa ya sintofahamu kwa waumini wa dini ya Ukiristo ambao wametafsiri kama udhalilishaji. Aidha,mamlaka imemtaka mmiliki wa wimbo huo Diamond kurekebisha maudhui ya video hiyo na pia kuomba watu na vyombo vya habari kutosambaza video hiyo.

MWAFRIKA AULA USEMAJI IKULU YA MAREKANI

Picha
Washington. Ofisi ya Rais wa Marekani imemtangaza bi Karina Jean-Pierre kuwa msemaji wa Ikulu ya Marekani yaani White House.Mwanamke huyu mweusi anachukua nafasi hiyo kwenye mamlaka ya juu kwenye serikali ya Marekani baada ya kuwa mtu wa karibu wa Rais Biden. Katika taarifa yake Rais Biden amemsifia kwa uzoefu,talanta na uadilifu akisema kwamba anajivunia kutangaza kuteuliwa kwake kama Katibu wa habari wa Ikulu hiyo huku msemaji wa sasa wa Ikulu hiyo Jen Psaki nae akiandika kwenye mtandao wake wa Twitter amemtaja Pierre kama mwanamke wa kwanza mweusi kushika wadhifa huo ndani ya Ikulu ya Marekani. Jean Pierre  mwenye umri wa miaka 44 amewahi kufanya kazi kwenye kampeni za Barack Obama mnamo mwaka 2008 na 2012 kabla ya kujiunga na timu ya Joe Biden 2020 ndani ya Ikulu ya Marekani.

KURASA ZA MAGAZETI LEO MEI 2

Picha
Habari ya kwako mpenzi mfuatiliaji wa ukurasa huu, hizi ni kurasa za magazeti hivi leo.