MANCHESTER CITY YAICHAPA 4 MAN UNITED

Manchester


Vilabu hasimu vya mji mmoja leo vimekutana kwa mchezo wa ligi ya EPL.Manchester United wakisafiri mpaka viunga vya Etihad wamekutana na kichapo cha magoli manne kwa moja (4-1).

Manchester City imejipatia karamu ya magoli kupitia Kelvin De bryune aliekwamisha magoli mawili (2) huku Mahrez nae akiingia kambani mara 2 na goli la mashetani wekundu likifungwa na Sancho "20.

Kelvin De'bruyne amepiga mashuti yake pekee kwenye lango la United mara 6 huku Manchester United ikipiga jumla ya mashuti 5.De bruyne amepiga pekee mashuti yaliyolenga goli 4 dhidi ya 2 za Man united na ametengeneza nafasi 5 pekee dhidi ya 2 zilizotengenezwa na Manchester United nzima.



Naye kocha wa Manchester City ,Pep Guadiola akuwa nyuma ni baada ya kusema hakuwahi kupata upinzani kama huo wa Manchester United leo kwenye kipindi chote cha kazi ya ukocha miaka 15 iliopita.


Maoni

HABARI KUU LEO

GUARDIOLA AWAPIGA DONGO LIVERPOOL

YANGA NA ARSENAL ZAGAWA DOZI