Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi 6, 2022

JINSI YA KUONGEZA KIPATO

Picha
Uchumi. Dunia ya leo ya mapinduzi ya nne ya viwanda ni tofauti na Dunia ya enzi za Ujima ambapo binadamu alitegemea kutembea kutafuta mahitaji yake kama matunda,mizizi na nyama kwa kuokota. Kwenye Dunia ya leo inakuhitaji kuwekeza katika maarifa zaidi ,ambapo utafungua akili na kuona fursa na kuziendea na pia utahitaji kuanza kuwekeza .Uwekezaji una maana pana ingawa watu wengi hufahamu uwekezaji ni pesa pekee ambalo sio kweli.Uwekezaji ni sawa na kumwambia Fundi wa nguo ashone suti,fundi akiambiwa suti yeye hupata picha kamili kwenye akili yake kwahiyo fundi mpaka anatoa hiyo nguo basi tunasema nguo inayoonekana ni picha ya kilichomo ndani ya fundi. Uwekezaji ni mawazo kwanza na ndio pesa hufuatia. Namna ya kuongeza kipato

MANCHESTER CITY YAICHAPA 4 MAN UNITED

Picha
Manchester Vilabu hasimu vya mji mmoja leo vimekutana kwa mchezo wa ligi ya EPL.Manchester United wakisafiri mpaka viunga vya Etihad wamekutana na kichapo cha magoli manne kwa moja (4-1). Manchester City imejipatia karamu ya magoli kupitia Kelvin De bryune aliekwamisha magoli mawili (2) huku Mahrez nae akiingia kambani mara 2 na goli la mashetani wekundu likifungwa na Sancho "20. Kelvin De'bruyne amepiga mashuti yake pekee kwenye lango la United mara 6 huku Manchester United ikipiga jumla ya mashuti 5. De bruyne amepiga pekee mashuti yaliyolenga goli 4 dhidi ya 2 za Man united na ametengeneza nafasi 5 pekee dhidi ya 2 zilizotengenezwa na Manchester United nzima. Naye kocha wa Manchester City , Pep Guadiola  akuwa nyuma ni baada ya kusema hakuwahi kupata upinzani kama huo wa Manchester United leo kwenye kipindi chote cha kazi ya ukocha miaka 15 iliopita.