Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi 5, 2022

CHELSEA YAICHAPA 4 BURNLEY

Picha
London Burnley wakisafiri kwenda mjini London kuifata timu ya Chelsea Fc wamepokea kichapo cha magoli manne bila majibu. Chelsea chini ya mkufunzi , Tomas Tuchel imejipatia magoli kupitia kwa     Reece James 47',Harvertz 52' 55" na Christian Pulsic 69". Urejeo wa James umeirejesha Chelsea kwenye makali yake maana winga huyo amefunga na kusaidia goli lingine. Chelsea wanasalia nafasi ya tatu nyuma ya Liverpool na Manchester city. Kwingineko, Liverpool imeichapa Westham goli moja kupitia kwa Sadio Mane. Matokeo mengine     Norwich 1-3 Brentford    Newcastle 2-1Brighton    Wolves 0-2 Crystal palace    Aston villa 4-0 Southampton

DRAKE ANUNUA NYUMBA YA NDOTO YAKE

Picha
Los Angeles. Rappa Drake wa nchini Marekani amenunua nyumba yenye thamani ya dola za marekani milioni 85 sawa na bilioni 187 za shilingi ya Tanzania. Nyumba hiyo iliyopo eneo la Beverly Hills mjini Los Angels nchini Marekani ina ukubwa wa futi za mraba 25,000 . Nyumba hiyo ina vyumba vya kulala 10,bafu za kuogea 22,gereji za magari 11,gym na viwanja vya mchezo wa tenisi.

RAIS PUTIN AOMBWA KUUA ZAIDI

Picha
  Moscow. Meja Jenerali wa Chechnya,  Ramzan Kadyrov  amemuomba Rais Vladimir Putin aruhusu mapigo mabaya ya kushtukiza ili Ukraine isalimu amri ndani ya muda mfupi wa masaa 24. Ramzan ambaye vikosi vyake viko vitani ameshauri kuachana na mapatano ambayo hayatakuwa na maana zaidi ya kusaini karatasi. Amesema hawezi kuvumilia kuona wanajeshi wake wanauawa na kadri wanavyozidi kuchelewa ndivyo wanakumbana na vikwazo zaidi.

Harmonize FT Bruce Melodie-TOTALLY CRAZY (Official Video)

Picha
 Msanii wa Bongo Fleva na mmiliki wa lebo ya KONDE GANG,Harmonize ametoa video ya wimbo wake aliomshirikisha Bruce Melodies hujulikanao kama "Totally Crazy). __ TAZAMA VIDEO

IRENE UWOYA ATOA SIRI YA KULA BATA

Picha
Dar es salaam. Mrembo Irene Uwoya amesema hafahamu ni kiasi gani cha pesa huwa anatumia kula bata? Mrembwende huyo akipiga stori Ijumaa hii amesema watu wanakuwa wanafatilia mtindo wa maisha yake ya kula bata. Mrembo huyu wa tasnia ya filamu Tanzania Bongo movie ametoa siri ya kula bata na kundi kubwa la watu anaosafiri nao nje na ndani ya nchi kwa kusema" pesa haitafutwi bali inategwa". Irene Uwoya ambaye kwa siku za karibuni amekuwa akitrend mitandaoni akila bata na watu wake pia na manunuzi ya magari ya thamani kubwa na matukio mbalimbali zikiwepo kumbukizi za kuzaliwa za watu wake wa karibu.

WATANZANIA WALIOKO UKRAINE WAPATA MSAADA

Picha
Moscow Balozi za Tanzania za Stockholm Sweden na Moscow Urusi zimesema serikali ya Urusi imeridhia wanafunzi wa kitanzania waliokuwemo kwenye mji wa Sumy nchini Ukraine, watumie mpaka wa Urusi ambao ndio upo karibu zaidi na mji huo. Zoezi la kutoa wanafunzi wote kutoka Sumy hadi mpaka wa Urusi litaratibiwa na serikali ya Urusi na tayari imeanza mpango wa utekelezaji . Wanafunzi wakifika mpakani ,ubalozi wa Tanzania nchini Urusi utakuwepo kwaajili ya kuwapa taratibu nyingine za kurejea nyumbani Tanzania.

KURASA ZA MAGAZETI LEO JUMAMOSI YA MACHI 5,2022

Picha
 Habari za magetini Leo jumamosi.

SIMBA YAICHAPA BIASHARA 3-0 LIGI YA NBC

Picha
Dar es salaam. Ligi ya NBC imeendelea leo ikizikutanisha timu za Simba Football Club na Biashara United  kwenye uwanja wa kumbukumbu ya hayati Benjamin Mkapa "Lupaso". Timu ya Simba ikitawala mchezo huo imeibuka na ushindi wa mabao matatu yaliyokwamishwa nyavuni na Sakho 8' , Mzamiru 13'  na Chama 18"  yote yakifungwa kipindi cha kwanza cha mchezo. Baada ya mchezo huo Simba imefikisha jumla ya alama 34 nyuma ya vinara Yanga wenye jumla ya alama 42. VIKOSI VYA TIMU ZOTE

SABABU ZA RAIS SAMIA KUKUTANA NA FREEMAN MBOWE

Picha
Rais wa Tanzania ,Samia Suluhu Hassan amekutana na mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA Freeman Mbowe. Rais , Samia ameeleza sababu za kukutana na Mbowe.