WATANZANIA WALIOKO UKRAINE WAPATA MSAADA

Moscow



Balozi za Tanzania za Stockholm Sweden na Moscow Urusi zimesema serikali ya Urusi imeridhia wanafunzi wa kitanzania waliokuwemo kwenye mji wa Sumy nchini Ukraine, watumie mpaka wa Urusi ambao ndio upo karibu zaidi na mji huo.



Zoezi la kutoa wanafunzi wote kutoka Sumy hadi mpaka wa Urusi litaratibiwa na serikali ya Urusi na tayari imeanza mpango wa utekelezaji .





Wanafunzi wakifika mpakani ,ubalozi wa Tanzania nchini Urusi utakuwepo kwaajili ya kuwapa taratibu nyingine za kurejea nyumbani Tanzania.


Maoni

HABARI KUU LEO

GUARDIOLA AWAPIGA DONGO LIVERPOOL

YANGA NA ARSENAL ZAGAWA DOZI