Machapisho

KURASA ZA MAGAZETI LEO MEI 16

Picha

SUAREZ ATANGAZA KUACHANA NA MADRID

Picha
Madrid, HISPANIA. Klabu ya Athletic Madrid imetangaza kuachana na mshambuliaji wake hatari Luis Suarez (35) baada ya msimu huu kuisha. Suarez ambaye mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu huu ,yeye pamoja na Hector Herrera wataondoka klabuni hapo na kupewa heshima zote za kuagwa na mashabiki katika uwanja wa  Wanda Metropolitan. Katika msimu wake wa kwanza na Athletic Madrid amefanikiwa kuchukua kombe la LaLiga na kufumania nyavu mara 21 katika mechi za LaLiga huku msimu huu tayari ashaweka kimyani magoli 11.

KURASA ZA MAGAZETI LEO MEI 15

Picha

KOFFI OLOMIDE AKUBALI UJIO WA WENGE

Picha
Kinshasa DRC Mwanamziki mkongwe barani Afrika Charles Antonio Mumba Olomide amefurahishwa na hatua ya wanamziki waliounda kundi la  WENGE MUSICA au WENGE MUSICA BCBG kuamua kuungana upya katika hatua ya kufufua kundi hilo.Kundi la WENGE MUSICA lilianzishwa na Didier Msika mwaka 1981 likipitia tena kwenye mikono ya JB MPIANA mnamo mwaka 1986 kablà ya kuvunjika mwaka 1997 huku sababu ikitajwa viongozi wake wakuu kutoelewana. Nguli huyu wa miondoko ya Sokous na Rhumba amesema anapenda kundi hili lirudi upya huku akizungumzia kile ambacho huwa kinatajwa kwamba yeye na Papa Wemba ndio walikuwa watu waliosababisha kundi hilo kufa amesema nafurahi sana WENGE MUSICA kurudi lakini mimi nilisemwa kuliua kundi hili lakini hiyo ilikuwa vita ya ushindani Wa kimziki na kutafuta ufalme pia wa mziki .