Machapisho

HISTORIA YA MAISHA YA PAPA WEMBA

Picha
Mwanamziki Papa Wemba alizaliwa 14 Juni 1949 na kufariki 24 April 2016,alizaliwa Lubefu Zaire ya Zamani. Papa Wemba ni mwamba Wa Mziki Wa Sukus na anafahamika Dunia kwa mtindo wake Wa uvaaji na utanashati ujulikanao kwa lugha ya Kifaransa yaani la Saperé. Umaarufu zaidi Wa Papa Wemba ulitokana na kundi lake la mziki la Viva la Musica  Mwaka 1969,Papa Wemba akiwa na hakina Nyoko Longo,Bimi Ombale,Moloko Leilei na Vuela Somo walikuwa vijana wa mwanzo watanashati na walijiunga na kuanzisha kundi la mziki la Zaiko Langa langa lililokuwa likiimba mziki Wa Sukusi.Tofauti ya mziki wa Sukusi na Rhumba la wakati huo wa makundi ya TP OK Jazz au Afriza International  ni kwamba mziki huu unaenda kasi mno.Mziki huu ulianzishwa na vijana waliochoshwa na mziki wa Rhumba wa kukumbatiana mwanzo mwisho bila jasho ,wao walitaka toka nukta ya kwanza ya kuanza mziki ni kucheza mwanzo mwisho. Sukusi  ni kizazi cha nne cha mziki wa Rhumba kutoka Zaire,utamaduni waliopitia vizazi vinne na kuunda kile kizazi k

KURASA ZA MAGAZETI LEO MEI 9

Picha

GUARDIOLA AWAPIGA DONGO LIVERPOOL

Picha
Manchester. Kocha wa Manchester City na raia wa Hispania Pep Guardiola ameipiga kijembe klabu ya Liverpool  kuwa haina uzoefu na kubeba kombe la ligi ya Uingereza kwasababu ndani ya miaka 30 wamebeba kombe moja. Pep ametoa kauli hiyo baada ya timu yake kuichapa klabu ya Newcastle kwa jumla ya magoli 5 na kukaa kileleni mwa ligi ya EPL kwa jumla ya alama 86 baada ya kuingia dimbani mara 35 sawa na Liverpool ambae anashika nafasi ya pili akiwa amekusanya alama 83. Aidha, Pep ameisifia Liverpool kwa kupambana vizuri kwenye ligi ya mabingwa ulaya yaani UEFA ambako tayari wako fainali pamoja na Real Madrid.

SIMBA YAICHAPA RUVU SHOOTING 4-1

Picha
Ligi kuu ya NBC imeendelea leo kwa kuzikutanisha timu za Simba sc na. Ruvu shooting stars kwenye dimba la hayati Benjamini Mkapa. Simba akiwa ni mwenyeji wa mchezo huo amemfunga Ruvu shooting magoli manne(4) kupitia kwa Kibu Denis,Raly Bwalya,John Bokko na Enock Inonga huku goli pekee la RUVU limefungwa na Haruna Chanongo. Katika michezo mitatu yaani ya Kombe la Azam na Ligi kuu , Ruvu imefungwa jumla ya magoli 14.Kwa matokeo ya leo sasa Simba Sc anafikisha alama 46 na michezo 22 akishikiria bado nafasi ya pili nyuma ya Yanga Fc mwenye alama 56 kwenye kilele cha NBC PREMIER LEAGUE. Aidha stori kubwa kwa mchezo wa leo ni goli la Nahodha wa Simba John Rafael Bokko ambaye amefunga goli lake la kwanza msimu huu.