ALIKIBA NA SHILOLE SASA NI DAMU DAMU
Dar es salaam.
Wasanii Alikiba na Shilole wameamua kumaliza tofauti zao baada ya kipindi cha miezi minne ya msuguano.
Wasanii Alikiba na Shilole wameamua kumaliza tofauti zao baada ya kipindi cha miezi minne ya msuguano.
Shilole ambaye ni msanii na mfanyabiashara alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya msanii mwenzake Alikiba kudai Shilole kuhudhuria kwenye shughuli yake bila kualikwa.Kauli hiyo ya Alikiba aliyoitoa akifanya mahojiano na kituo kimoja cha redio jijini Dar es salaam ilimuibua Shilole alietokwa na maneno mazito aliyoyapost kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram.
Shilole na Alikiba wamekubali kurudi kwenye ukaribu wao wa zamani ni baada ya mwana mama Shilole kusema yeye na Alikiba wamemaliza tofauti zao kijeshi.
Maoni