ZARRI ATISHIA KUWASHTAKI WANAOMCHAFUA MITANDAONI
Johannesburg.
Zarri the bosslady ameonya wale wote ambao wanatumia jina lake mitandaoni kuwashtaki.Hii inajiri baada ya mwanamziki na mwanamitindo wa Marekani Cardi B kumshinda mzalishaji wa maudhui kwenye mtandao wa youtube kwenye kesi iliolindima kwenye mahakama moja nchini Marekani.Kwenye hukumu ya kesi hio imeamriwa mshtakiwa kumlipa Cardi B zaidi ya bilioni 7 za Tanzania.
Kufuatia mkasa huo wa Marekani nae Zarri ametumia mwanya huo kuwaonya wote wanaotumia jina lake vibaya kwenye mitandao ya kijamii.
Maoni