BASHUNGWA ATAKA HALMASHAURI ZOTE KUWA NA MASTER PLAN

Dar es salaam.




Waziri wa nchi ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na serikali za mitaa Innocent Bashungwa ametaka halmashauri zote nchini kuwa na master plan na sio tu halmashauri zenye miradi ya maendeleo pekee.



Bashungwa ametoa maelekezo hayo wakati akipokea taarifa za TSCP,ULGSP na DMDP kutoka kwa kikundi kazi kilichokuwa kinasimamia fedha za mkopo kutoka Benki ya Dunia ambazo zimetumika kwenye ujenzi wa barabara za mijini na vijijini zilizo chini ya TARURA.



Waziri Bashungwa amesisitiza ya kwamba ni lazima halmashauri ziweke mipango ya maeneo kabla hili mabadiliko ya technolojia na saikolojia yasije kuleta changamoto katika mipangilio ya maeneo.


Haya yanajiri wakati waziri Bashungwa akiwa katika ziara yake katika mkoa wa Dar as salaam.


Maoni

HABARI KUU LEO

GUARDIOLA AWAPIGA DONGO LIVERPOOL

YANGA NA ARSENAL ZAGAWA DOZI